Social Icons

Tuesday 28 January 2014

SOMO MUHIMU LA LEO: FAHAMU JUU YA BIASHARA YA MTANDAO , JIKOMBOE SASA NA WEWE KUANZA BIASHARA HIYO, SOMA HAPA



BIASHARA YA MTANDAO:
Biashara ya mtandao ni biashara inayozaa na kuzalisha, ni biashara ya kuambiwa, kukubali, kutumia, na kuwaambia wengine, ili nao wafanye kama ulivyofanya wewe yaani uwaambie, wakubali, watumie nao wawaambie wengine. (DUPLICATION)
Leo nazungumzia biashara ya mtandao kwa kuwa watanzania wengi kama bado hawajaielewa hivi na walioielewa kama wanapotosha hivi baadhi yao.


Utakuta unatoa darasa au unamuelezea mtu kuhusu biashara ya mtandao anakuja si ile kama kampuni Fulani, huo ni unafiki sio kujua huko, kama uliskia kaa kimya mbona hukuanza wewe.  Msikilize anayetoa mada tena katika wakati na sehemu inayoeleweka, kwanini naongea haya, kwa kuwa utakuta wengi wa watu hawa kabla hujaendelea anaanza kuelezea kampuni ingine na kuanza kuiponda au kuisifia, ingawa wengi utasikia ya nchi gani hiyo, hamna lolote mimi nimeshatumia sana.

Biashara ya mtando ilianzishwamiaka ya 1960s huko Marekani na mamilionea wengi wa marekani walianza kushika milioni yao ya kwanza kwa kupitia Biashara hii ya mtandao.

Kwa hapa kwetu Tanzania makampuni yanazidi kuja mengi na biashara hiyo inazidi kushika kasi kwa nguvu kutokana na wengi wanavyoonja mafanikio.
ukisikiliza watu wanavyoifanya biashara hii utakata tamaa na kuitwa machinga lakini kiuhakika na ukweli biashara hii haipaswi ubebe bidhaa uzunguke nazo kama machinga.  Wengi tumeshindwa kuelewa biashara hii na ndio maana mtu akifanya baada ya miezi mitatu au minne anahisi haoni mafanikio mwisho anaamua kuacha na kusema biashara hailipi, wakati anafanya biashara hii kimakosa
Jinsi ya kufanya hii biashara ni kama nilivyosema ambiwa, kubali, tumia, muambie na mwingine, akubali, atumie naye amuambie na mwingine.
Ili ufanikiwe katika biashara hii ni lazima kwanza uijue kampuni, mwenye kampuni, bidhaa zake, na mfumo wa biashara yenyewe.  Biashara hii ni ngumu sana lakini wagumu ndio watakao baki.  Tuna ushahidi wa wafanyabiashara wengi wa biashara hii ya mtandao ambao wanapata kipato kikubwa mwisho wa mwezi, na mwisho wa mwaka, wapo wanaopata hadi shilingi milioni 10 kwa mwezi, na mwisho wa mwaka wanapata zaidi ya shilingi milioni mia mbili na zaidi (TSHS. 10,000,000 hadi 200,000,000) kama ulikuwa hujui jua kuanzia leo.  Biashara hii ukiisikiliza unaweza kwenda kukopa mabilioni ya shilingi ili uje upate yale yote unayoambiwa katika kampuni ile, ni kweli wayasemayo yanapatikana hakuna mjadala, hakuna tapeli hata kampuni moja katika zilizopo Tanzania, tatizo ni wafanyabiashara wameelewa muundo wa biashara hiyo? 

Wanajua jinsi ya kuwatafuta wateja? Je kuna idadi gani ya watanzania walio na afya njema, kuna idadi gani ya watanzania wanaoumwa, na je kuna idadi gani ya watanzania wanaoumwa huku hawatambui kama wanaumwa.
Angalia taarifa hii ilitoka mwaka jana katikati yaani 2013, inasema hivi katika watu bilioni saba (7,000,000,000) dunia 5% wana afya njema nao wana umri wa miaka kuanzia 0 hadi 5 je wewe unayesoma umo humu kwenye hili kundi?.  20% ni wagonjwa waliolazwa Muhimbili, na  Hospitali nyingine unazozijua ndani na nje ya nchi pia na wale wanaotumia dawa kwa kutambulika.  Na 75% ni wagonjwa watarajiwa au wanaotembea na ugonjwa pasi na kujua na ndio maana utakuta wengi wetu tuna kufa ghafla maana tuna magonjwa huku tunatembea na huku akili zetu nafsi zetu zikitundanganya kuwa ni wazima wa afya.  Nikuulize swali! Lini ulisikia kitu kama radi kimepiga upande wa kushoto ukashtuka ukakimbilia hospitali?  Na lini gari yako imelia kitu mvunguni tiii au umesikia mvumo huuelewi ukakimbia kwa fundi? Acha unafiki jibu ukweli.  

Huo ukweli wako ndio utakuponya.
Kama nilivyosema biashara hii ilianza miaka ya 60, sisi ndio inaingia sasa Tanzania ndio maana tunashtuka hatuzijui vizuri kampuni hizi wala biashara hii, na bahati mbaya biashara hii ya mtandao imekuja Tanzania na makampuni ya virutubisho mengi au yote kuliko ya vifaa kama sufuria, umeme na kadhalika.  Wenzetu walio endelea hukimbilia sana biashara hii kwa kuwa inalipa vizuri sana, huku kwetu hasa Tanzania tunaikimbia kwa kuwa ni ya kujituma.

Biashara ya mtandao inajenga asikuambie mtu, unajua mambo mengi kuliko unavyodhani, wala usitangulize dharau kuwa hawa ni wamachinga sijui wanaongea sana hapana, tena biashara ya mtandao hutakiwi kuwa muongeaji sana, unatakiwa kuwa mtumiaji sana wa bidhaa ili wengine waone mabadiliko yako nao watamani kutumia bidhaa unazotumia, ili nao wawe kama wewe.

KOSA KUBWA TUNALOFANYA WAFANYABIASHARA WA MTANDAO
Unaposikia au unapoitwa katika kampuni ngeni au wewe ni mgeni katika kampuni ile basi kuna wale wenyeji wanaokujua na kukuita pale basi hukuita kichwa, jembe kwa kuwa wanaamini ukiingia utawabuzuta watu wajiunge na ile kampuni kwa kuwadanganya mambo yasiyo ya kweli na kweli ili waingie na mwisho wakiingia hawaoni ulicho maanisha kwa kuwa hayo uliyosema si ya kuonekana leo ni hadi miaka mitatu hadi mitano, na kosa lingine ni kitendo cha kuanza kupiga hesabu kichwani eheeee nimeambiwa kuna dawa ya kisukari nina shangazi ana kisukari, mjomba ana kisukari, jirani ana kisukari, fulani ana matatizo ya hedhi, mama fulani ni mnene sana, mama ndimu, ana vidonda vya tumbo, bi mkora ana pressure, shekiangio ana tatizo la ngozi baaasi watakoma naenda kila mmoja anipe shilingi laki nne nimpe full dozi, sasa utakuta mwana mtandao anaenda kwa wateja wenye hela ili apate bonus, na points za mwezi bila kuangalia biashara hii haitaki wagonjwa kwa asilimia kubwa, biashara hii inataka mtu atumie virutubisho hivi kwa kuwa vyakula tunavyokula, maji na juice na pombe tunazokunywa zina sumu, pia dawa karibu 90% zina kemikali hivyo tunatakiwa kutumia hivi virutubisho ili kuondoa kemikali hizo.

Sasa hivi kila chakula kila tunda, kila mboga inawekwa dawa, au mbolea zina dawa, hivyo ni vyema kujifunza vyema bidhaa hizo ili kuweza kutafuta wateja wa kujiunga na kuzitumia kwa mafanikio, tatizo sio kampuni na wala tatizo si nchi tatizo ni sisi wasambazaji, tukitulia na kujifunza vizuri tutaisaidia sana jamii.

Hospitalini ni sehemu ya kikinga maradhi, lakini sasa hivi ni kinyume, hospitalini ni sehemu ya kutibu magonjwa tena yaliyoshindikana, elimu hizi ambazo zinatolewa na makampuni ya virutubisho ilitakiwa itolewe na manesi na madaktari ili watu wasifikie hatua ya kuumwa, figo, kuto kupata choo, moyo, macho, ngozi, kutokupata hedhi, ulaji bora wa chakula bora, unywaji wa maji, unywaji wa sharubati, utumiaji wa mboga za majani na kadhalika. Haya yote yanatakiwa kufanywa na hospitali, lakini pongezi kwa wafanyabiashara wa biashara ya mtandao wanafanya kazi kubwa sana kuelimisha jamii, ingawa jamii yenyewe nayo kuelewa ni kazi sana, lakini naamini wataelewa tu.

BIASHARA YA MTANDAO INAIINGIZIA SANA SERIKALI MAPATO
Kama ulikuwa hujui basi biashara ya mtandao inaiingizia sana serikali mapato, maana kampuni inapoingia nchini inafuata taratibu zote za kisheria, za ulipaji kodi na inapewa TIN namba na inaingia katika usajili wa ulipaji wa kodi kisheria.  Ukitaka kujua hili zaidi nitafute nikupeleke ukaone.

WAFANYABIASHARA YA MTANDAO WANAKOPESHEKA
Unapojiunga katika kampuni yoyote ya biashara ya mtandao unajisajili na kuweka vielelezo vyako vyote katika fomu, na pia kampuni inakutambua kuanzia katika nchi yako hadi dunia nzima ambapo kampuni hiyo ipo, kwa kuwa unapofikia cheo fulani basi kuna kamisheni unapata kutokana na cheo chako na wale wenzako mlio katika cheo kile katika dunia nzima, hivyo gawio la pato la mwezi huo linagawiwa kwa ninyi mameneja wote duniani.  Vile vile unapopanda cheo kimoja kwenda cheo kingine kampuni itakutambua na kukupa cheo chako na dunia nzima itakutambua kwa kufikia hatua hiyo.  Sasa nauliza mabenki yaliyopo hapa Tanzania kuna siku mlishawaza kuwafuata wafanyabiashara wa mtandao na kupata darasa kuhusu biashara hii inayoingiza mamilioni ya shilingi hapa nchini kila siku? Je ikiwa sisi wafanya biashara wa mtandao tunatambulika nje ya Tanzania kwa nini benki iliyopo Tanzania isinitambue? Naomba sana watu wa benki kama mnataka faida kubwa nioneni mimi niwaoneshe wapi mnalosa wateja wengi wenye pesa nyingi na wanaokopesheka na wenye uwezo wa kulipa halafu ninyi hamuwafuatilii.  Biashara yoyote ambayo mfanyabiashara anaweza kupata kuanzia shilingi 100,000 nadhani anakopoesheka bila matatizo kikubwa ni kufuata taratibu, kanuni na sheria za mikopo.
Naamini ikiwa benki zitatutambua na kutuamini tunaweza kukopa na kufanya biashara zetu na kurejesha mikopo kwa wakati, kikubwa kinachotakiwa ni kupeana elimu tu.
Imani yangu wanamtandao tukijiunga vikundi vya watu kuanzia 30 kama vicoba tunaweza kupata mikopo mikubwa na kufanya mambo makubwa sana katika biashara hii.

Nakuomba mdau unayesoma hapa kama utakuwa hujaelewa na una swali usisite kunipigia simu, kutuma sms, au email ambazo zinaonekana katika mawasiliano hapo ili tupeane mawazo zaidi.
Hii ndio ajira ya karne ya 21, inakupa uhuru wa muda, uhuru wa pesa, uhuru wa kustaafu unavyotaka.
Pesa zipo hapa!

No comments:

Post a Comment

Asante kwa ku Comment yako ujumbe wako ni muhimu