Social Icons

Tuesday 11 February 2014

SOMO LA LEO: JIFUNZE JUU YA AJALI ZA MOTO,KUJIKINGA NA KUTUMIA VIFAA VYAKE



AJALI YA MOTO NA VITENDEA KAZI VYAKE

Ni kitu gani husababisha moto?
Swali hili ukimuuliza mtu yeyote asiye na ufahamu na moto hatakuwa na jibu sahihi.
Chanzo cha Moto ni moto wenyewe, hili ndio jibu halisi.
Kuna aina nyingi za moto;
1.      Moto wa Umeme
2.      Moto wa Mlipuko
3.      Moto wa kuanzishwa na Mtu
4.      Moto Unaozuka Wenyewe kutokana na mlundikano wa vitu, kama majani na vitu vingine
5.      Na Kadhalika

Wengi wetu hatufuatilii kuhusu elimu hii ya moto tukiamini wapo wanaozima moto, lakini naomba nikuambie mdau wa blog hii, hakuna kazi ya mtu mmoja katika majanga hasa ya moto.  Huwa tunawalaumu sana Kikosi cha Zimamoto kwa kuwa huwa hatujui ni adha gani wanaipata, ingawa mimi nawalaumu kwa upande mwingine kuwa ilibidi hata wangekuwa wanakwenda kama wanasiasa katika majukwaa kwa kutoa matangazo kuwa siku Fulani tarehe Fulani, saa Fulani tutakuwa sehemu Fulani tutatoa elimu kuhusu majanga ya moto.  Hii yote ni kujaribu kutapakaza elimu hii adimu ya kujiokoa na kuokoa katika ajali za moto wa aina yoyote.  Heri wananchi wengi wapate kitu kidogo watakacho ambulia kuliko walivyo sasa hawana uelewa wa kitu chochote kile.
Je ni mwananchi gani wa kawaida anajua jinsi ya kutumia fire extinguisher, ni aina gani ya fire extinguisher itatumika katika moto wa uliosababishwa na shoti ya umeme, na ni fire extinguisher gani itatumika katika moto uliosababishwa na mafuta, ni fire extinguisher gani itatumika ikiwa moto umesababishwa na moto kutoka jiko la mkaa ukarukia nguo, ukaenda katika godoro au makuti na kuwaka.
Je ikiwa mtu katika ajali ya moto, nguo zake zimeshika moto labda mgongoni atatakiwa kufanya nini kabla ya yote, je mtu akiona moto unawake tangu awali anatakiwa kufanya nini kabla ya kupiga simu kituo cha zimamoto na kutoa taarifa zilizo sahihi ili zimamoto waje na gari husika kwa moto husika.  Maana sio kila gari ya zima moto inazima moto wowote.
Je wakati unapambana na moto unajilindaje na moto unaopambana nao?  Amini usiamini moto una akili sana, na ndio maana tunasema kupambana na moto sio kuzima moto, moto unauwezo wa kukuchungulia na kukusoma ulivyo kwa wakati huo na kukushambulia kama hujui, moto una shambulia kwa malengo, kama hutakuwa makini moto unakuua mara moja.  Ni haki yako mtanzania kujua jinsi ya kupambana na moto mdogo hadi mkubwa, wa majumbani hadi misituni.  Tambua vifaa vyote au vichache vya kuzuia na kuzima moto.  Ni hatari sana utakuta tunaishi katika majumba hatuna hata sehemu za kukimbilia kama kutatokea tatizo la moto, nyumba hazijakaa kitaalamu sana, likitokea la kutokea na grills tunazoweka siku hizi hatoki mtu ndani.  Nyumba tunajenga bila malengo, hakuna anayewaza janga la moto.  Ndio moto hutokea mara moja kwa miaka kadhaa ila hiyo siku moja inakurudisha sifuri kabisa kama hukuwa na kitu.  Ni wangapi tuna bima za nyumba labda, ni wangapi tuna bima za maisha, zaidi ya bima ya gari tena kwa kuwa utakamatwa na trafiki barabarani, na bima yenyewe tunakata third party mnaita.  Kama nilivyosema blog hii itakuwa inakukumbusha au kukupa kitu kipya ambacho unakijua lakini hukifuatilii na huna hata wazo nacho, lakini kikitokea ni lawama lawama kwa kila mmoja kuona anaongea sahihi kumbe tatizo tunalo katika jamii huku.
Leo mimi nitakufundisha kidogo sana kuhusu kuzima moto kwa kutumia ile mitungi ya kuzimia moto fire extinguishers’

Wenyewe fire au zimamoto wana maneno yao wanaita PASS
P = PULL (ONDOA PIN)
A = AIM (ELEKEZEA MPIRA WA KUZIMIA KATIKA MOTO SIO KATI MWANZO)
S = SQUEEZE (BINYA ULE MKONO WA KURUHUSU MAJI AU UNGA KUTOKA)
S = SWEEP (PELEKA MKONO WAKO WA KUSHOTO KULIA NA KUSHOTO)

Mtungi ule hushikwa na mkono wa kulia, na ule mpira wa kuzimia hushikwa na mkono wa kushoto, wanaposema toa pin sio pin number, kuna pin utaona imewekwa kwaajili ya kuzuia maji au unga uliomo ndani ya mtungi yasitoke au usitoke.  Angalia mazingira ya moto ulipoanzia halafu elekezea ule mpira wa mtungi sio katikati ya moto, utaungua na hutakuwa unafanya kitu, anza kupambana nao kama unaanza kula sambusa hivi, pembeni pembeni hadi unajua chanzo, pia soma upepo unakotoka na kuelekea, kwa kuwa ukipingana na upepo utacheza pata potea.  Moto huwa unakaa upande ambao wewe ni kikwazo kwako, wakati wewe unatafuta hewa wenyewe unaichukua ile hewa na kukupa wewe wakati mgumu.  Ukishajiweka katika mazingira mazuri ya kutambua hayo yote basi pambana nao.
Na kama ni ndani ya jingo kumetokea moto na ni lazima ufungue mlango ili utoke ndani ya korido, unashauriwa usifungue kwanza mlango hadi uhakikishe kuwa moto haujafika mlangoni, kwa sasa majengo mengi ya mjini ni magorofa, yana miundo tofauti na nyumbani, ikiwa unataka kutoka kwanza gusa mlango kama unaupima joto, kwa style ya kama unampiga mtu kibao cha kerebu, maana huko ndio kuna hisia nzuri za kitu, ukihisi joto sana usifungue maana utakutana na moto ambao utakuua,na utasababisha oxygen kuingia kwa wingi katika chumba hivyo utauita moto kwa nguvu sana.
Hakikisha unafuata taratibu zote bila ya kupiga kelele au kuchanganyikiwa kwa kuwa unapofanya hayo utapoteza nguvu na utabaki katika moto, tafuta EXIT sehemu za kutokea ili ujikwamue. 
Ikiwa bahati mbaya moto umekushika mgongoni lala chini haraka, kisha jigeuzegeuze ili uuzime, usikimbie huku unapiga kelele utakuwa unazidi kuuchochea na utaungua vibaya.
Nakuomba kuanzia leo hakikisha popote unapokaa pawe na njia ya kukimbilia ikiwa itatokea janga la moto.  Epuka kujaza maganda ya Apples (Tufaa) sehemu moja, au makaratasi mengi au majani mengi sehemu moja kwa muda mwingi hivi husababisha moto bila kiberiti, ndio maana unaweza shangaa msituni moto unaanza tu bila mtu kuuwasha, na wengi wetu huhisi mtu katupa kichungi cha sigara, si kweli kwa asilimia kubwa, majani nayo ni chanzo kizuri cha moto.
Kuna vitendea vingi vya kuzuia na kuzima moto;
1.      Mitungi ya kuzima moto (Fire Extinguisher)
2.      Magari ya kuzima moto
3.      Ndege za kuzima moto
4.      Meli za kuzima moto
5.      Treni za kuzima moto
6.      Ndoo zenye mchanga wa kuzima moto
7.      NK
Ukiingia katika mitaa yetu hutaona hata sehemu moja yenye bomba la maji ya kuzima moto Hydrants kitu ambacho ni hatari sana, na ndio maana hata wale zimamoto wakifika eneo la tukio wakaanza kupambana na moto maji yaakiisha huondoka na kwenda mbali kujaza maji tena, na foleni na miundo mbinu yetu hii wakirudi wananchi wanakuwa na hasira na kuongea maneno ya hatar hatari wakati hawatambui wale zimamoto ni shida gani wanapata kwa wakati ule.  Inatia huruma sana.
Nakushauri msomaji ukimaliza kusoma hapa ukikutana na mtumishi wa Zimamoto mhoji maswali mawili matatu ili uweze kupata kitu kipya kwake na kitakachokusaidia siku moja.
Unapojenga nyumba jitahidi kuweka eneo maalumu la usalama, pia jitahidi na Inspekta wa zimamoto apitie mchoro wako wa nyumba yako na afike kuhakiki kama umefuata maelekezo katika ujenzi wako.
 
Labda nikuambie au nikupe darasa dogo kuhusu ile mitungi Fire Extinguishers;
KUNA AINA 6 ZA MITUNGI AU TAMBUA MITUNGI HII TOFAUTI YAKE
1.      WATER (UNA KIKARATASI CHEKUNDU [COLOR CODE RED])
2.      WET CHEMICAL (COLOR CODE YELLOW
3.      FOAM (COLOR CODE BLUE)
4.      POWDER (COLOR CODE WHITE)
5.      CARBONDIOXIDE (COLOR CODE BLACK)
6.      POWDER (COLOR CODE YELLOW)
Vile vile hii mitungi imegawanyika katika makundi 6 tena ya matumizi;
Kuna A, B, C, D, E, na F
A.    Wood paper and plastics
B.     Flammable and Combustible Liquids
C.     Flammable Gases
D.    For Fire Including Combustibles metal use special purpose extinguisher
E.     Electrically, Energized Equipments
F.      Cooking Oils and Fats
Hili somo ni kubwa sana linahitaji uelewa na mapenzi ya dhati kabisa kwako.
Okoa maisha yako na ya wengine, kuwa balozi mzuri wa kupambana na majanga ya moto

Swali sasa, kwa mimi, wewe, pamoja na Serikali tumejiandaaje na majanga ya moto kuanzia majumbani, maofisini, vituo vya mafuta, hospitali, shuleni, misikitini, makanisani, viwanjani, katika majumba ya starehe, misituni, maporini na popote pale ambapo janga litatokea.  Jukumu la kutoa elimu hii ni la idara husika ikishirikiana na wizara na serikali kwa ujumla, wananchi tuna haki ya kimsingi kujua jinsi ya kutumia zana hizi, kutambua zana hizi.  Nasi wananchi tukifundishwa tuyashike yale mafunzo ili iwe rahisi kwa lolote litakapotokea.  Kubwa zaidi likitokea janga tusikimbilie kuangalia tutapata madhara makubwa kwa kushangaa kuliko matarajio yetu.

No comments:

Post a Comment

Asante kwa ku Comment yako ujumbe wako ni muhimu