Social Icons

Tuesday 11 February 2014

HUU NDIO UVUVI WA KISASA , SOMA HAPA UPATE KUELEWA


Habari ndugu msomaji wa blog hii.

Uvuvi katika nchi yetu hii ya Tanzania unachukuliwa kama utani, unachukuliwa kama mtu akishindwa maisha basi anaingia majini na kwenda kuchukua samaki na kuleta nchi kavu ili wateja tununue.

Uvuvi wa samaki ni kazi tena kazi yenye kipato kikubwa sana katika dunia hii.  Wengi wa wavuvi wetu wanawaza kuchukua mitumbwi na kuanza kupiga makasia kwenda baharini kuvua samaki, lakini sidhani kama kuna wanaokaa na kufikiria kununua meli  kubwa zenye uwezo wa kubeba tani mia mbili na hamsini na kuendelea za samaki kwa siku.  Samaki wenye minofu na wanaotakiwa katika soko ni ni wale walio katika kina kirefu na umbali mrefu ambao boti zetu hizi tunazotumia haziwezi kufika, na hata zikifika huko basi hawawezi kumudu nguvu za maji hayo.

Uvuvi wa kusafiri umbali mrefu na meli kubwa zenye uwezo mkubwa ni njia pekee ya kumnyanyua mvuvi katika uvuvi wake wa samaki, kuna samaki wengi wanaotakiwa katika soko.  Soko ninalo zungumzia hapa ni la ndani na la nje ya nchi.

Ikiwa meli itakuwa na uwezo wa kubeba tani 200 basi kuna uwezekano wa kutengeneza kiasi kikubwa cha fedha kila siku katika uvuvi.  Ikiwa wale samaki walioitwa wa Magufuli walikuwa tani 296.32 wenye thamani ya shilingi bilioni 2.07. ina maana wale samaki walikuwa kila kilo ni shilingi 7,000.
7,000 kwa kilo.  Chukua meli ina tani 296.32, tani moja ni kilo 1,000 x 296,320 = bilioni 2.07 je wale samaki tunaovua pale ferry, na msasani wanafika bei hii kwa siku au wiki? Kama ndio basi wavuvi wamelogwa, kwanini hawaendelei?
Mada hii naiandika nikiwa nawaza kwa uwezo wangu, je kwanini mdau wewe usiidadavue biashara hii ukaona kama inalipa tujiunde kama kikundi kikubwa tununue hata meli moja kubwa (30.2m longline fishing vessel) ambayo ni kama shilingi za kitanzania milioni 500 meli inaweza kuingiza bilioni 2 kwa wiki, hatuoni kuwa tunapoteza muda sana?
Ikiwa wadau 100 tutachanga shilingi 5,000,000 tutapata kiasi cha shilingi 500,000,000 ambacho tunaweza kuagiza meli hii na kufanya taratibu nyingize za kisheria na tukaanza rasmi kazi ambapo meli hii hata kama itaingiza shilingi bilioni 2 kwa mwezi ina maana kwa miezi 12 tutakuwa na shilingi bilioni 24 sasa hapo mdau utakataa kuwa mmoja wa wawekezaji wa meli hii, na hapo tunaweza nunua meli 4 zaidi ambazo zitakuwa zinafanya kazi kwa masoko yote ya samaki.  Samaki watakuwa wakubwa wenye bei rahisi na si visamaki vidogo vya bei ghali tena samaki watazaliana sana kwa kuwa wale wakubwa ndio watakao fuatwa.  Tunaona wavuvi wengi sana wanavamia sehemu za mazalia ya samaki hii inachangia hata kupotea kwa samaki hata katika misimu yao.  Huwezi kupiga vita kuvua samaki kwa net ikiwa wavuvi wana waza leo, kesho Mungu atajua, ni lazima tuwe na mawazo mapana ili tuweze kutokea upande wa pili wa mafanikio.
Serikali inakosa mapato makubwa, wavuvi wanakosa kipato kikubwa, wateja wanakosa samaki wenye ladha na ubora kwa kuwa hakuna vitendea kazi, manahodha wapo wengi meli chache, ikiwa kundi litanunua meli 4 kuna ajira 4 za manahodha, na mabaharia, wavuvi kwa nafasi zao, hapa tutakuwa tumetengeneza ajira pia.  Tutakuwa tumeongeza kipato kwa nchi, kipato kwa familia na kadhalika.


Mdau hebu kaa chini ufikiri halafu utoe mawazo yako hapa.

No comments:

Post a Comment

Asante kwa ku Comment yako ujumbe wako ni muhimu