Social Icons

Monday 10 February 2014

NI KWELI HAIWEZEKANI KUWA NA SHIRIKA LA NDEGE BINAFSI? SOMA HAPA





SHIRIKA LA NDEGE BINAFSI
Ndugu mdau wa Buberwa Robert Blog,
Najaribu kukupa kitu ambacho nakiwaza kichwani kwangu, kichwa change kimejaa mambo mengi sana ambayo huwa nashindwa kuelewa, je hatuna watu wanao waza, wapo lakini ni mambo magumu, mfumo wetu ni wa kusubiri serikali ifanye nasi tukosoe au kushangilia pale jambo linapoenda kinyume na matarajio ya wananchi?

Leo naomba niongelee kuhusu usafiri wa anga kwa kuanzisha kampuni yetu ya usafiri wa anga itakayoitwa vyovyote wadau watakavyoamua, shirika litakalokuwa na malengo ya kusafirisha abiria ndani ya Tanzania yaani mikoa yote, nje ya Tanzania ikiwa na maana ya Afrika nzima na dunia.  Tutafanyaje hadi tuweze kutokea hadi nje huko duniani, ni mipango ya shirika litaloongozwa na wasomi wenye ueledi wa hali ya juu na si wale ambao kila kitu kwao hakiwezekani.  Ikiwa wenzetu wanaweza kwa nini sisi tushindwe ikiwa tuna saa 24 wote, miaka sawa, tunavuta hewa moja, dunia ni moja ambayo iko katika mfano wa duara, wao dunia yao haipo flat kwanini tushindwe?

Ndugu mdau unayesoma hapa, ninataka utoe mawazo ambayo yatakuwa na tija kwako, kwangu, kwa Yule na wale na Tanzania nzima, leo naongea hili kama ndoto lakini siku likitimia kila mmoja atajisifia, leo hii tunasoma lakini masomo yetu yanatutengeneza tuwe nani, kwanini hatuwi wabunifu, na ubunifu wenyewe uwe wa kuzalisha ajira, kuzalisha fedha, kuzalisha utaalamu na si kusoma na kuzurura na bajasha ukitegemea kuajiriwa, mimi nasema ni aibu kwa msomi mwenye elimu ya juu kutembea na bahasha eti anatafuta ajira, hiyo elimu yako unataka uitumie kwa kufungwa kwa kupangiwa muda wa kazini, mpango kazi usio na tija kwako na familia yako, unawafaidisha waajiri tu ndani ya miaka yote unayofanya kazi.

Leo nakuja na mada ya kufikirika lakini inayowezekana ikitendewa kazi, na si kuidharau na kuona huyu jamaa anawaza nini mbona hiki kitu kigumu, unajua maendeleo yanaletwa na wewe pale unapowaza maendeleo, na si kulalamikia maendeleo yaletwe na mwingine.
Hivi umeshawahi kuwaza kununua ndege labda aina ya Boeing 777 ambayo inauzwa dola za kimarekani 76 milioni, bei ya chini ambapo tunaweza kuwaza kuchanga kwa kiwango chetu na kuchukua mikopo pia ikiwezekana ili tuweze kuanzisha kampuni yenye hata ndege 10 kwanza, ikiwa ndege 2 kubwa za kutoka nje ya nchi jirani, na ndege 8 ndogo za abiria kuanzia 6 hadi 60 zitakazokuwa zinakwenda mikoani kila siku kwa bei nafuu?
 
Wengi wetu tunasomesha watoto, sisi tumeshafubaa, kwanini tusitengeneze kampuni kubwa ya usafirishaji wa anga, kampuni ambayo itaaminika ndani na nje ya nchi kwa huduma bora?  Huwa hatuna mawazo haya zaidi ya kutaka kupinduana kisiasa tu kila siku?  Nina hakika kama tuna hasira na maendeleo basi tunaweza tengeneza ajira za vijana walio wengi tena watoto wetu wenyewe na sio wageni ambao watakuja kuchukua hadi senti ya mwisho,  sikatai kuna sehemu lazima wataalamu wan je waingie lakini waingie kwa mkataba ambao utatutengenezea watanzania wataalamu kama ao katika vyuo vikuu vya duniani huko ambavyo vitawaamini wasomi wetu.
Kuna huduma nyingi za anga, kama kusafirisha abiria, kusafirisha mizigo, kusafirisha wagonjwa, kuzima moto, kuchukua picha, huduma za kilimo, huduma za hali ya hewa na mambo mengine ambayo yanawezekana.
Kila mara huwa naongelea suala la kujiunga na kutengeneza kitu kikubwa chenye maana kwa wananchi hiki kitu kama kweli tutafunga macho na kweli kuamua kuwekeza tunaweza kufanya jambo kubwa sana katika nchi hii,  Shirika letu litatakiwa kuwa na kiwango kisichopungua dola za kimarekani zaidi ya 10 trilioni ili kuweza kuanza angalau kwa ndege chache ndogo na kubwa.

Najua mdau unayesoma hapa una maswali mengi kuhusu jambo hili lakini kama tutakaa na kujadili na wataalamu wakaanza kuandaa Business Plan na tukafanikiwa kuanza kuchanga na mambo mengine ninaamini hili shirika linaweza kuanza na kila mmoja wetu akaja kujisifia sana huko mbele ya safari.  Tutatakiwa kujua, faida, hasara kwa upande wa fedha, usafirishaji, abiria au wateja kwa kuingia katika biashara sio kwa kulikatalia kichwani.

Siku zote ukijipa majukumu mazito utafanikiwa, lakini ukiyaachia majukumu kwa wengine huwezi kuendelea kwa kuwa maendeleo yanakutegemea wewe ili yaendelee.  Kumbuka wenye mawazo si lazima wawe wasomi, na watendaji si lazima wawe wenye fedha, bali kila mmoja anamtegemea mwenzake kwa jambo moja ama lingine.  Tushirikiane ili tuijenge Tanzania yenye mafanikio na si malalamiko


Hivi naeleweka?

No comments:

Post a Comment

Asante kwa ku Comment yako ujumbe wako ni muhimu