Social Icons

Monday 3 February 2014

KWA WALE WENYE MIILI MIKUBWA: HIVI NDIVYO UNAWEZA KUJUA UMEPUNGUZA UZITO WAKO KIASI GANI KWA WIKI.







MTU ANAWEZA KUPUNGUZA UZITO KIASI GANI KWA WIKI?

Mtu anaweza kupungua kilo ngapi kwa wiki ni swali ambalo watu wengi hujiuliza.Hasa pale wanapotaka kuanza harakati za kupunguza uzito. Ni wazi kwamba watu wengi hupenda kufanya Diet za muda mfupi na wapate matokea makubwa ya haraka. (umeula wa chuya, umeutengeneza huo uzito miaka mingapi unataka upungue kwa dakika ngapi?)
Kiasi cha uzito unaoweza kupunguza kwa wiki hutofautiana kati ya mtu na mtu.  Ingawa nia na juhudi binafsi huchukua nafasi kubwa katika hili, kuna mambo mengine yanayoleta tofauti hizo;
1. Jinsi
2. Umri
3. Ukubwa wa mwili
4. Vyakula unavyokula
5. Mazoezi unayofanya
Nguvu joto za chakula (kalori)
Nguvu za chakula yaani kalori, (calories) ni kiasi cha nguvu ambacho hupatikana au hutolewa na chakula kifikapo mwilini. vyakula vyote  vinaidadi fulani ya kalori isipokua maji tu ambayo hayana kalori.
Kalori hufanya kazi mwilini kama ambavyo mafuta aina ya petroli au dizeli hufanya kazi kwenye gari. Ili gari iweze kutembea lazima mafuta yaungue ili kutoa nguvu ambayo hutumika kutembeza gari,na jinsi unavyozidi kutembea ndivyo ambavyo mafuta huzidi kuungua hadi kwisha.
Mwili wa binadamu nao hufanya hivyo hivyo, nguvu unazopata kwenye chakula yaani kalori, huungua ili kutoa nguvu ambayo inauwezesha mwili wako kufanya mambo mbalimbali kuanzia kupumua, kutembea, kukimbia,na yote ambayo mwiili hufanya.  Kadiri unavyofanya shughuli nyingi zitumiazo nguvu ndivyo ambavyo kalori hupungua mwilini.
Nusu kilo ( 1/2 kg) ni sawa na kalori 3500.  Ili upunguze nusu kilo katika uzito wako nilazima utoe kalori 3500 katika mwili wako. Unaweza kutoa  kalori hizo katika mwili wako  kwa kupunguza kiasi cha kalori unazokula kwa siku au kwa kuongeza mazoezi au kufanya kazi zinazofanya utumie nguvu nyingi ili utumie nguvu za ziada ambazo mwili wako umetunza (unene wako)
Kupunguza kalori (chakula) ni muhimu zaidi kuliko kufanya mazoezi hasa kwa mtu mwenye nia ya kupunguza uzito.  Pia mtu anayepunguza uzito haraka zaidi endapo atapunguza kiasi cha kalori anazokula na kufanya mazoezi ya mwili ili kuunguza kalori ambazo mwili wake umetunza.

TOFAUTI
Jinsi ya mtu huchangia katika kuamua ni kiasi gani cha uzito anaweza kupunguza kwa wiki. Kwa kawaida wanaume wanamisuli mingi kuliko wanawake. Utafiti unaonesha kwamba misuli hutumia kalori nyingi hivyo uwepo wake katika mwili hufanya mtu aweze kupunguza uzito haraka. Hii hufanya wanaume waweze kupunguza mwili kwa haraka kuliko wanawake.
Pia tafiti hizo huonyesha kwamba mtu mwenye uzito mkubwa ana uwezo wa kupunguza uzito kwa haraka zaidi kuliko  mtu mwenye uzito mdogo, hasa mwanzoni anapoanza kupungua.
MAZOEZI

Kiasi cha kalori unachoweza kutoa mwilini unapofanya zoezi au shughuli nyingine hutokana na uzito wa mtu. Mtu mwenye uzito mdogo hutoa kalori chache na mwenye uzito mkubwa hutoa kalori nyingi kwa kiasi kilekile cha mazoezi.
Mfano:mtu mwenye kilo 72.5 atatoa calories 986 kwa kukimbia kwa dakika 60, lakini mwenye kilo 108 atatoa calories 1,472 kwa kukimbia dakika hizohizo 60
Kadiri unavyotoa  kalori nyingi mwilini ndivyo uzito unavyozidi kupungua
DIET
Diet kali hulenga kumfanya mtu apunguze uzito mwingi ndani ya muda mfupi. Tafiti huonyesha kwamba asilimia kubwa ya uzito unaopotea unapofanya diet kali ni uzito wa maji mwilini.

Ni  ngumu sana kwa mwili kutoa kilo 1 ya mafuta mwilini kwa wiki.  Hata hivyo endapo utaendelea na diet kali kwa muda mrefu basi unaweza kupunguza mafuta ya mwili na hivyo kupunguza mwili kwa haraka.
Ukifanya diet kali sana ,ambayo inakufanya uingize kalori chache sana mwilini basi kuna uwezekano wa kupunguza kilo ndani ya muda mfupi.

MAGONJWA NA MATIBABU

Historia ya afya yako ni Sababu nyingine inayochangia katika kujua kiasi cha kilo unachoweza kupunguza kwa wiki.  Magojwa yasababishwayo na homoni za mwili hufanya iwe ngumu sana kupunguza uzito wa mwili.

Tafiti zinaonyesha kwamba baadhi ya madawa kama madawa ya kisukari na dawa za uzazi wa mpango hufanya  iwe ngumu kupunguza uzito. Baadhi ya madawa pia hufanya mtu ashindwe kabisa kupunguza uzito na madawa mengine hunenepesha mwili.


USHAURI
Endapo umekua ukifanya mazoezi na diet kwa muda mrefu na hupungui uzito, ni vyema ukamuaona Daktari wako na kumuelezea hali hiyo ili aweze kutafuta chanzo cha tatizo hilo na kulitafutia ufumbuzi.
Kama unafanya juhudi za kupunguza uzito basi punguza kiasi cha kalori unazokula kwa siku na pia fanya mazoezi ili kuunguza kalori za akiba mwilini.
HITIMISHO.
Naamini umeelewa nikwanini hakuna kipimo maalumu cha kiasi cha uzito ambao mtu anaweza kupunguza kwa wiki, kwani vigezo vyote hivi huchangia katika kupungua.
Hata ivyo vitu kama msongo wa mawazo na kutokupata usingizi wakutosha, pia huweza kuchangia mtu kupungua uzito au kuongeza uzito.

Tukutane tena ili tupeane darasa la tiba mbadala 

Huna sababu za kutumia madawa ....

No comments:

Post a Comment

Asante kwa ku Comment yako ujumbe wako ni muhimu